Akiba ni muhimu sana katika harakati za kutafuta maisha,ukizungumza na watu mbalimbali ukawauliza juu ya kuweka akiba utapata majibu mengi,Mwingine atakwambia kwamba "pesa napata lakini haitoshi .Ukijenga utamaduni wa kujiwekea akiba utajikuta pesa yako inatosha.Kuweka akiba sio lazima uwe na kipato kikubwa bali hicho kidogo ukijiwekea mikakati stahiki utaweza kuweka akiba ya kutosha Hizi no mbinu ambazo kwa namna moja ama nyingine zitakuwwzesha kuweka akiba 1:kuwa na nidhamu ya fedha Hili ni suala dogo kulifanya lakini ni gumu sana kulitimiza.Fedha yoyote inahitaji nidhamu unatakiwa kuheshimu kila senti unayoipata,epuka matumizi yasiyo ya lazma maana pesa ukiwa nayo itakuongoza kufanya kila jambo maana kwa wakati huo unaona pesa unayo.In bora ukipata pesa weka akiba angalau asilimia kumi kuliko kuitumbua bila mpangilio 2: jiwekee malengo yanayopimika Watu wengi hasa wa kipato cha kati na cha chini huwa hawajiwekei malengo...
Ndugu msomaji na mfuatiliaji wa Habarika.com blog nipende kukwambia kwamba kuna biashara nyingi sana duniani.Leo tunazungumzia sifa za biashara inayoweza kukupa mafanikio makubwa.Kimsingi biashara yoyote utakayoamua kufanya kama utakuwa serious nayo ukavumilia na ukajikita hasa inaweza kukulipa lakini kama utaingia kwenye biashara kwa mguu mmoja ( kwa kubeep) bila shaka haitakupa mafanikio mwishowe utakata tamaa ufunge biashara yako.Zifuatazo ni sifa za biashara zenye mafanikio makubwa 1: biashara iwe na urahisi wa kueleweka,ili biashara yako izae mafanikio na kukua zaidi inatakiwa iwe inaeleweka kwa wateja wako na watu wote kwa ujumla kwa urahisi. 2: biashara iwe na wateja wa kujirudiarudia Biashara yoyote yenye watteja wa namna hiyo haiwezi kufa na itazidi kukua kwasababu aliyenunua Jana atarudi leo na kesho na wewe utaendelea kuuza kila siku na kupata faida. 3: Sifa ya tatu ni hii,biashara iwe na bidhaa zisizo...
Comments
Post a Comment